Sonzaschool
Rudi

Sekondari ya Juu · Kidato cha Tano

Kiswahili 1

Kauli za kiswahili

takriban dakika 2 kusoma

Majadiliano
Mada za sehemu hiiMatumizi Ya SarufiMada 7

Kauli za kiswahili

Kauli ya Kutenda

  1. Hueleza jambo lililotendwa na mtenda.

  2. Kiambishi tamati: -a

  3. Mfano:

    • gand-a
    • pig-a
    • som-a

Kauli ya Kutendwa

  1. Hueleza kuwa mtu/vitu wametendewa jambo.

  2. Alomofu: -w-, -liw-, -lew-

  3. Mfano:

    • pig-w-a
    • sem-w-a
    • chom-w-a
    • o-lew-a
    • vu-liw-a
    • ambi-w-a

Kauli ya Kutendewa

  1. Huonyesha mtu ametendewa jambo kwa niaba yake.

  2. Alomofu: -iw-, -ew-, -liw-, -lew-

  3. Mfano:

    • lim-iw-a
    • chez-ew-a
    • som-ew-a
    • kimbi-liw-a
    • zo-lew-a
    • va-liw-a
    • chomo-lew-a

Kauli ya Kutendea

  1. Tendo limefanyika kwa manufaa/faida ya mwingine.

  2. Alomofu: -i-, -e-, -li-

  3. Mfano:

    • pig-i-a
    • lal-i-a
    • ruk-i-a
    • chez-e-a
    • zo-le-a
    • o-le-a

Kauli ya Kutendesha

  1. Huonyesha mtu anavyosababisha mwingine kutenda jambo.

  2. Alomofu: -ish-, -esh-, -lish-, -lesh-, -sh-, -z-

  3. Mfano:

    • imb-ish-a
    • kimbi-z-a
    • tembe-z-a
    • pit-ish-a
    • ru-sh-a

Kauli ya Usababishaji (Kutendesha)

  1. Huonyesha wasababishi wa tendo kutokea kwa mhusika mwingine.

  2. Alomofu: -esh-, -lesh-, -lish-

  3. Mfano:

    • og-esh-a
    • zo-lish-a
    • ka-lish-a
    • va-lish-a
    • shon-esh-a
    • som-esh-a
    • chem-sh-a

Kauli ya Kutendana

  1. Hushirikisha wahusika wawili kutendeana kwa pande zote mbili.

  2. Alomofu: -an-

  3. Mfano:

    • pend-an-a
    • suk-an-a
    • sukum-an-a
    • sem-an-a
    • ruki-an-a

Kauli ya Kutendeana

  1. Mhusika wa kwanza hutenda kwa niaba ya mwingine na kinyume chake.

  2. Alomofu: -an- kati ya mzizi na kiambishi tamati.

  3. Mfano:

    • suk-i-an-a
    • sem-e-an-a
    • som-e-an-a
    • zo-le-an-a
    • va-li-an-a
    • o-le-an-a

Kauli ya Kufungamana (Kutendana maalum)

  1. Huonyesha watu/vitu kukaa pamoja kwa muda mrefu.

  2. Alomofu: -am-

  3. Mfano:

    • ung-am-a
    • ach-am-a

Kauli ya Kinyume cha Kutenda

  1. Huonyesha kinyume cha tendo (kubatilisha).

  2. Alomofu: -o-, -u-

  3. Mfano:

    • umb-u-a
    • teg-u-a
    • chom-o-a
    • kunj-u-a
    • pang-u-a

Kauli ya Kishikanishi (Kutendana maalum)

  1. Huonyesha mshikamano au kushikana kwa vitu/watu.

  2. Alomofu: -at-

  3. Mfano:

    • pak-at-a
    • kam-at-a
    • fumb-at-a

Mwalimu

Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.

Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.

Ingia ili kuuliza

Majadiliano

Hakuna maswali bado

Ingia ili kuuliza
Inapakia majadiliano…