Mada za sehemu hiiTungoMada 2
- Sentensi
- Kuchanganua Sentensi
Uchanganuzi wa Sentensi
Kuchanganua sentensi ni mbinu ya kuigawa sentensi katika sehemu mbalimbali ambazo huunda sentensi hiyo.
-
Kutaja aina ya sentensi yaani kama ni sentensi sahili, ambatano au changamano.
-
Taja sehemu zake kuu yaani; kiima na kiarifu (kishazi) au KN na KT (kimuundo)
-
Kama ni sentensi sahili onyesha vipashio vya kiima na kiarifu; yaani jina, vivumishi, vitenzi, shamirisho na chagizo n.k
Kama ni sentensi changamano taja vishazi vyake na kazi ya kila kishazi tegemezi katika hiyo sentensi changamano yaani taja: kama kishazi tegemezi kinavyovumisha jina au KN kilicho katika kiima au KN cha kishazi huru. Mfano; Mzee uliyemwona jana ni baba yangu.
"uliyemwona jana" ni kishazi tegemezi kivumishi kinachovumisha jina "mzee" lililo kiima cha kishazi huru (K/H) "mzee ni baba yangu"
-
Kutaja aina za maneno yote yaliyomo katika sentensi hiyo.
Mfano; Baba na mama wanakula ugali
N t N T N
-
Kuandika tena sentensi
Kuna njia kuu nne za uchanganuzi wa sentensi
- Matawi/ ngawe/ michoroti
- Jedwali/ visanduku
- Mishale/ mistari
- Sentensi/ maelezo/ maneno
Mfano;
Mwalimu mwema amemsaidia mwanafunzi
Mbuzi aliyenunuliwa juzi amechinjwa leo asubuh

Mfano;
Gari lililopinduka jina limeinuliwa na dereva wake amefariki dunia
S. ambatano
Wanafunzi waliimba wimbo wao vizuri sana

Mfano;
Shangazi anasoma kitabu polepole
Shangazi anasoma kitabu polepole
Mbwa aliyepata kichaa mwogope
Mbwa aliyepata kichaa mwogope
Juma anacheza mpira na Damasi anasoma kitabu
- Hii ni sentensi ambatano.
- Sentensi hii ina sentensi mbili na kiunganishi.
Sentensi ya kwanza ina kiima na kiarifu:
- Kiima kina jina.
- Jina ni Juma.
- Kiarifu kina kitenzi na nomino.
- Kitenzi ni anacheza.
- Nomino ni mpira.
- Kiunganishi ni na.
Sentensi ya pili ina kiima na kiarifu:
- Kiima kina jina.
- Jina ni Damasi.
- Kiarifu kina kitenzi na jina.
- Kitenzi ni anasoma.
- Jina ni kitabu.
Balozi wetu ni mtu jasiri sana
Hii ni sentensi sahili.
Sentensi ina kiima na kiarifu:
- Kiima kina jina na kivumishi.
- Jina ni balozi na kivumishi ni wetu.
- Kiarifu kinakitenzi kishirikishi + Kirai nomino.
- Kirai kielezi
- Kitenzi kishirikishi ni ni.
- Kirai nomino kina jina na kivumishi:
- Jina ni mtu na kivumishi ni sana.
Mwalimu
Unasoma somo hili? Niulize nikuelezee chochote kilichomo.
Ingia ili kumuuliza Mwalimu wa AI wa Sonza kuhusu mada hii.
Ingia ili kuulizaMajadiliano
Hakuna maswali bado